More about me...

My photo
Kilifi, Coast, Kenya
Informing is not only my profession but also passion

Welcome

Welcome

Wednesday, 6 August 2014

Harambee Stars yapata kocha mpya



Shirikisho la kandanda nchini Kenya FKF limeteua wanachama wapya wa kamati ya kiufundi ya timu ya taifa Harambee Stars.

Akihutubia wanahabari hapo jana katika hoteli moja jijini Nairobi, mwenyekiti wa FKF Bw. Sam Nyamweya alimtaja (aliyekuwa) kocha wa klabu ya Gor Mahia Bobby Williamson kama mkufunzi mpya wa Harambee Stars. Nahodha wa zamani wa timu hiyo Musa Otieno ndiye kocha msaidizi huku Simon Muluma akikabidhiwa wadhifa wa meneja mkurugenzi.

Hatua hii imeafikiwa siku mbili tu baada ya raia wa Ubelgiji Adel Amrouche kutimuliwa kama kocha wa Harambee Stars kufuatia matokeo duni ya timu hiyo. Amrouche pamoja na wanakamati wote wa kiufundi waliachishwa kazi siku ya Jumapili, muda mchache tu baada ya timu hiyo ya taifa kupoteza nafasi ya kufuzu kwa michuano ya taifa bingwa barani Afrika. Timu hiyo ilitoka sare tasa na timu ya taifa ya Lesotho katika mechi ya marudio baada ya kupoteza 1-0 hapo awali kwenye mechi ya kwanza.

Bobby Williamson alikuwa mkufunzi wa timu ya taifa ya Uganda, Uganda Cranes, kwa muda wa miaka mitano kabla ya kuteuliwa kusimamia Gor Mahia mnamo Julai mwaka jana. Katika msimu wake wa kwanza, Williamson aliiwezesha timu hiyo kutwaa ubingwa wa ligi kuu nchini Kenya.